Marehemu Askofu mstaafu Fortunatus Lukanima kuzikwa Kagunguri, Jimbo Katoliki la Bunda
Waamini pamoja na watu wenye mapenzi mema nchini Tanzania wanaendelea kuomboleza kifo
cha Askofu mstaafu Fortunatus Lukanima wa Jimbo Katoliki Arusha, kilichotokea kwenye
Hospitali ya Rufaa Bugando, Mwanza, Jumatano tarehe 12 Machi 2014 kwa Ibada ya Misa
Takatifu na Rozari Takatifu.
Ratiba elekezi ya maziko inaonesha kwamba, Alhamisi
tarehe 13 Machi 2014 majira ya jioni, Waamini wa Jimbo kuu la Mwanza wanaadhimisha
Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kanisa kuu la Tokeo la Bwana, Jimbo kuu la Mwanza. Ijumaa
tarehe 14 Machi 2014, majira ya asubuhi, kutakuwa na Ibada ya Neno la Mungu katika
Hospitali ya Rufaa Bugando na baada ya hapo, msafara utaanza safari kuelekea Kagunguri,
Kisiwani Ukerewe, Jimbo Katoliki la Bunda.
Wakiwa Nansio, waamini wataadhimisha
Ibada ya Misa Takatifu majira ya mchana na baadaye kutakuwa na mkesha wa Sala kwenye
Kanisa la Kagunguri, moja ya Makanisa Mama Jimbo kuu la Mwanza kwa wakati huo.
Ibada
ya Misa Takatifu kwa ajili ya Mazishi ya Askofu mstaafu Fortunatus Lukanima, yatafanyika
Jumamosi, tarehe 15 Machi 2014, majira ya asubuhi. Ni Ibada inayotegemewa kuhudhuriwa
na waamini wengi kutoka Jimbo kuu la Arusha, Jimbo kuu la Mwanza na Jimbo Katoliki
la Bunda. Apumzike kwa Amani.