Onesho la Picha za hija ya Papa Paulo VI mjini Yerusalemu
Viongozi wa Makanisa ya Kikristo mjini Yerusalemu wamefungua onesho la picha kati
ya Patriaki Anathegoras wa Kanisa la Kiorthodox la Costantinopoli na Papa Paulo VI
walipokutana, wakasali na kuzungumza pamoja, miaka 50 iliyopita. Hizi ni picha zinazonesha
hotuba na zawadi zilizotolewa na Papa Paulo VI alipotembelea Nchi Takatifu.
Haya
yote ni maandalizi ya hija ya kichungaji ya Baba Mtakatifu Francisko katika Nchi Takatifu
atakaoifanya mwishoni mwa Mwezi Mei, 2014, kama sehemu ya Maadhimisho ya Jubilee ya
Miaka 50 tangu Papa Paulo VI alipokutana na kuzungumza na Patriaki Anathegoras wa
Costantinopoli, katika harakati za kujenga na kudumisha majadiliano ya Kiekumene miongoni
mwa Wakristo.