Askofu Mkuu mteule Megan ateuliwa kuwa Balozi wa Vatican nchini Sudan
Baba Mtakatifu Francisko amemteua Monsinyo Hubertus Matheus Maria Van Megen kuwa Balozi
mpya wa Vatican nchini Sudan pamoja na kumpandisha hadhi kuwa ni Askofu mkuu. Askofu
mkuu mteule Megen alizaliwa kunako tarehe 4 Oktoba 1961 huko Eygelshoven. Baada ya
masomo na majiundo yake ya Kikasisi, akapadrishwa kunako tarehe 13 Juni 1987.
Askofu
mkuu mteule ana shahada ya uzamivu katika Sheria za Kanisa. Alianza utume wake katika
masuala ya kidiplomasia mjini Vatican kunako tarehe Mosi, Julai 1994. Amewahi kutekeleza
utume wake nchini Sudan, Uruguay, Brazil, Yerusalemu, Slovachia; Ofisi za Mwakilishi
wa kudumu wa Vatican kwenye Umoja wa Mataifa zilizoko Geneva na hatimaye, Malawi.