2014-03-07 11:25:18

Rufuku ya biashara ya silaha bado ipo nchini Somalia


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kauli moja limepitisha azimio linalopiga rufuku biashara ya silaha ndogo ndogo nchini Somalia hadi kufikia tarehe 25 Oktoba 2014. Rufuku ya Umoja wa Mataifa dhidi ya silaha kubwa na nzito itaendelea kufanyiwa kazi na kwamba, Serikali ya Somalia inawajibu wa kimaadili kuhakikisha kwamba, azimio hili linatekelezwa kikamilifu.

Serikali ya Somalia ilikuwa imeliomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuondoa rufuku ya biashara ya silaha ili kuiwezesha Somalia kujizatiti katika masuala ya ulinzi na usalama kwa raia na mali zao dhidi ya vitendo vya kigaidi nchini humo.







All the contents on this site are copyrighted ©.