Papa - Kipindi cha Kwaresima ni wakati sala, kufunga na kutubu.
(Vatican )Katika Kipindi cha asubuhi Jumatano, Baba Mtakatifu Francisko alitoa Katekesi
yake kwa mahujaji na wageni kama ilivyo kawaida kwa siku hii. Mafundisho ya Papa
yalikubusha kwamba, Jumatano hii ni Jumatano ya Majivu, ambamo Wakristu wote wanakianza
kipindi cha siku arobaini za safari Kwaresima, ambacho huongoza katika maadhimisho
ya Siku Tatu Kuu za Pasaka” Triduum” , kumbukumbu ya mateso , kifo na ufufuo wa Bwana,
kiini cha fumbo la ukombozi wa Kristu kwa biandamu wote.
Papa ameutaja wakati
huu kuwa ni wakati muhimu, ni wakati wa kupiga hatua ya nguvu ya mageuzi kiroho, akimtaka
kila Mkristu, kufanya mageuzi ya kutoka nje ya tabia na mazoea mabaya, ovu na udanganyifu.
Aliongeza katika kipindi cha Kwaresima , Kanisa linatoa mialiko mawili muhimu: kwanza
kuwa na ufahamu zaidi juu ya kazi ya ukombozi ya Kristo , kuishi na dhamira zaidi
kwa mujibu wa ubatizo wetu.
Ufahamu katika maajabu ya Bwana aliyoyafanya kwa
ajili ya wokovu wetu, ambayo yanagusa akili na mioyo yetu, katika kujenga tabia ya
kutoa shukrani kwa Mungu kwa ajili ya neema zake anazotupatia, kwa kuwa yeye alitimiza
yote, kwa ajili ya watu wake na ubinadamu wote. Na hili linakuwa ni sababu ya sisi
kufanya mageuzi chanya kiroho, kama jibu la kushukuru maajabu ya fumbo la upendo
wake wa kukomboa.
Papa ametaja wito wa pili wa Kanisa katika kipindi hiki,
ni kufanya mabadiliko na kutembea katika ukweli wa njia Ubatizo, katika maana kujinasua
na mazoea mabaya yenye kudhoofisha mwendo katika safari ya kukutana na kutembea pamoja
kama jumuiya, Parokia na kama taifa. Papa ameasa na kuomba uangalifu dhidi ya pinzani
na mashinikizo ya tamaduni, yanayoweza kuwa kikwazo au kuwa kinyume na kumcha Mungu.
Mashinikizo ya kidunia yanayofanya hata wazazi kupata ugumu wa kufundisha watoto
wao faida za kumcha Mungu, kushindwa kufundisha hata ishara ya msalaba.
Maisha
ambayo uhalifu wa vita,madhulumu, umaskini na matendo mengine maovu dhidi ya jamii
yamegeuzwa kuwa jambo la kawaida. Papa alieleza na kukumbuka vurugu na ghasia za
mapigano , zinazosikika kila siku katika vyombo vya habari, ambazo zinasababisha mateso
kwa watu wake kwa waume. Watu wanao lala mitaani, ambao hawana tena makazi . Watu
walio lazimika kuwa wakimbizi, wale wanao tafuta uhuru na heshima yao, inayokataliwa
kama vile si haki msingi.
Papa aliendelea kusema, tumekuwa na mazoea ya kuishi
katika jamii isiyojali uwepo wa Mungu, yenye kujidai inaweza kuishi bila Mungu na
tabia zingine mbovu zisizo kuwa za Kikristo, ambazo hulewesha moyo na matamanio ya
starehe za kidunia.
Hivyo kwa Mkristo, kuwadia kwa kipindi hiki cha Kwaresima,
unakuwa ni wakati wa unaoongoza katika kufanya mageuzi ya kweli ,ni wakati wa kufanya
mabadiliko katika kukabiliana na hali halisi za uovu, kama changamoto katika maisha
ya kumfuata Kristu. Ni wakati wa kufanya mabadiliko ya kuonekana, kwa mtu binafsi
na jamii kwa ujumla, kupitia njia ya kuiamini Injili na Mungu. Kwa njia hii pia inaruhusu
sisi kuangalia kwa macho mapya, mahitaji ya ndugu zetu wahitaji. Kwaresima ni wakati
mwafaka kwa kubadilika na kumpenda jirani yako , upendo wenye kufahamu majitoleo na
ukarimu wa moyo na kwa huruma wa Bwana, anayetuimarisha sisi kwa umaskini wake"
(cf. 2 Kor 8.9 ). Ni wakati wa kutafakari juu ya fumbo hili, kati imani , upendo
, msalaba na ufufuo wa Kristo , tukiwa na utambuzi kwamba, wokovu huu ni zawadi isiyo
na kipimo, inayotolewa bure kwetu na mpango wa Mungu.
Papa alikamilisha
kwa kutaja mambo muhimu mengine ya kukumbuka katika kipindi hiki cha Kwaresima kwamba,
ni pamoja na kumtolea Mungu shukurani kwa ajili ya fumbo hili la upendo wake kusulubiwa,
imani ya kweli , yenye kufanya mageuzi na kuufungua moyo wa kuwaona ndugu wengine
wahitaji. Kwa njia hii, Papa aliomba msaada wa Mama Bikira Maria, Muumini wa kwanza
katika Kristo, aungane nasi, wakati huu wa siku za maombi ya nguvu na toba , ili
tupate kujitakasa na kufanya upya wa kiroho, katika kuliamini Fumbo kuu la Pasaka
ya Mwanae.