2014-03-05 09:25:33

Msalaba daima ni njia ya Mkristu : leo hii kuna wafia Ukristo wengi kuliko awali.


(Vatican Radio) Mahubiri ya Baba Mtakatifu Francisko , katika Ibada ya Misa ya mapema asubuhi siku ya Jumanne katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta- Vatican, yalilenga zaidi katika mateso ya Wakristo katika jamii ya kisasa. Aliwataka Wakristu kukumbuka kwamba, Ukristu daima ni kuwa tayari kuubeba Msalaba, kama njia ya kumfuata Kristo. Leo hii kuna Wakristo wengi wanaoifia imani yao kwa Kristo, kuliko wakati miaka ya kwanza ya Kanisa.

Katika hotuba yake , Papa alirejea somo la Injili ambamo Petro anamwuliza Yesu, nini wanafunzi wake, watapewa kwa kumfuata. Papa alieleza pengine Petro alidhani kwamba kumfuata Yesu itakuwa shughuli kubwa ya kibiashara kwa sababu Yesu ni mkarimu, lakini daima Yesu aliwaonya, malipo ya kumfuata, daima yataambatana na mateso.

Papa Francisko aliendelea kuonya kwamba, Msalaba upo daima katika njia ya ukristo! Na kwamba, kanisa litakuwa na waamini wengi katika jumuiya za Kikristo na wengi wao watapambana na mateso. Hii ni kwa sababu dunia haivumilii utakatifu wa Kristo. Haivumilii kusikia Neno la injili. Havumilii kuziishi Heri . Na hivyo wale wanaomkiri Kristo wanapambana na mateso : kwa maneno, na vitendo , kama ilivyokuwa kwa Wakristo wa karne ya kwanza , walishutumiwa vikali, kufungwa na kuuawa

Lakini bahati mbaya binadamu husahau, Papa alieleza huku akifanya rejea kwa Wakristo wengi wa miaka 60 iliyopita, waliodhulumika katika makambi ya kazi , katika makambi ya jeshi dhalimu la Nazi, makambi ya Wakomunisti n.k. Na hivyo ndivyo hata leo hii...kuna mashahid wengi zaidi wafia Ukristu , kuliko hata nyakati za karne ya kwanza ya Kanisa. "


Papa Francis alisema kuwa kuna ndugu wengi na waume kwa wake , ambao wanateseka kwa kumshuhudia Kristo katika maisha yao ya kila siku.. Baadhi hawawezi kubeba Biblia mikononi mwao barabarani.
Wanashutumiwa nakuwekwa hatiani kwa kosa la kuwa Biblia . Hawawezi kuvaa msalaba . Papa anasema hii ndiyo njia ya Yesu. Lakini ni barabara furaha kwa sababu Bwana wetu kamwe hatuweki katika majaribu yaliyo zaidi ya uwezo wetu . Maisha ya Kikristu si kwa sababu za faida za kibiashara , wala si ajira , lakini ni jambo jepesi la kuamua kumfuata Yesu. Na ndivyo inavyotokea katika kumfuata Yesu.

Papa ameeleza na kuhimiza Wakristu kujenga ndani hamu ya kuwa jasiri katika kumshuhudia Yesu, kwamba ni jambo jema leo hii kwa Wakristo wote wake kwa waume. Papa aliangalisha mawazo yake kwa wale wasiokuwa na fursa ya kusali pamoja, kwa sababu kufanya hivyo ni makosa , wale ambao hawawezi kuwa na kitabu cha Injili au Biblia kwa sababu ni kosa kuwa na vitabu hivyo.

Papa alikamilisha kwa kuwakumbuka pia wale ambao hawawezi kwenda Misa kwa sababu ni haramu nakutoa mwaliko kwa Wakristo kujiuliza iwapo wako tayari kubeba msalaba na kuteseka, mateso kama Yesu alivyofanya? Ni vizuri kwa kila mmoja wetu kwa kufikiri juu ya hili , alihitimisha.








All the contents on this site are copyrighted ©.