2014-03-05 14:31:27

Gustavo Andùjar Robles kutoka Cuba achaguliwa kuwa Rais wa SIGNIS duniani


Mkutano mkuu wa SIGNIS uliokuwa unafanyika mjini Roma kuanzia tarehe 25 Februari hadi tarehe Mosi, Machi 2014 kwa kuwashirikisha wajumbe 300 kutoka katika nchi 80, wamemchagua Gustavo Andùjar Robles kutoka Cuba kuwa ni Rais mpya wa SIGNIS, ambalo ni Shirikisho la Wanahabari Wakatoliki Duniani. Wajumbe wamepata pia fursa ya kupitia Katiba Mpya ya SIGNIS iliyopitishwa hivi karibuni na Baraza la Kipapa la Walei.

Rais Mpya wa SIGNIS amewataka wajumbe kujifunga kibwebwe ili kuweza kukabiliana na changamoto zinazoendelea kujitokeza katika ulimwengu wa utandawazi na maendeleo ya sayansi na teknolojia ya habari. SIGNIS inapaswa kuwa na mwelekeo mpana zaidi katika kukabiliana na changamoto hizi.

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa maadhimisho ya Mkutano mkuu wa SIGNIS mjini Roma, aliwataka Wanahabari Wakatoliki kusimama kidete ili kupambana na changamoto za daima, ili waweze kutangaza hekima, ukweli na uzuri unaofumbatwa katika Injili ya Kristo.

Viongozi wengine walioachaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa SIGNIS ni:
Frank Frost kutoka Marekani.
Lawrence John kutoka Malaysia.







All the contents on this site are copyrighted ©.