2014-03-04 14:56:13

Ujumbe wa Papa Francisko kwa Maaskofu wa Hispania : dumuni katika utume wa Kanisa.


(Vatican) Papa Francis Jumatatu alikutana na Maaskofu Katoliki wa Hispania, wanapo endelea na hija yao ya kitume ya ad Limina Visita , katika Idara za Vatican. Papa akikutana nao kwa ujumla,hotuba yake, ililenga zaidi katika hali ya sasa ya Kanisa nchini Hispania na dunia ya magharibi kwa ujumla.

Aliwaambia, kwa wakati huu, wanapoteswa na ugumu wa wabatizwa wengi kutojali sheria na kanuni za kanisa, ni lazima kutafuta mbinu za kukabiliana na utamaduni wa kidunia , unao shinikiza maisha ya kidini kuwa ni maisha binafsi , na kutaka kumtoa Mungu katika mazingira ya umma. Ni lazima watafute mbinu za pamoja kuonyesha jinsi ilivyo muhimu kwa mtu kutosahau historia yake. Hivyo kutokana na hilo, wanapaswa kufundisha kwa ujasiri kwamba, neema ya Mungu kamwe haiwezi kusitishwa na utendaji wa biandamu, na kwamba, fadhila za Roho Mtakatifu zina endelea kufanya kazi hata katika hali halisi za sasa.

Baba Mtakatifu aliwahimiza Maaskofu kuidhaminisha imani yao kwa Roho Mtakatifu, kupandikiza mbegu ya imani thabiti katika mioyo yao wote, walio kabidhiwa katika huduma yao ya kichungaji .

Papa alitia shime dugu zake katika Kristo na katika utumishi wa Kanisa , kutoachia mwanya wowote kwenye jitihada za kufungua njia mpya kwa ajili ya maisha ya Kiinjili, yaifikie mioyo ya watu wote , ili waweze kugundua kile ambacho tayari kimehifadhiwa ndani ya Kristo kama rafiki na ndugu .

Aliwataka Maaskofu hao kuyaweka Makanisa yao katika hali ya Utume wa Kudumu, kwa ajili ya kusaidia kuimarisha imani , hasa kwa watoto, na kurejesha tena kanisani wale waliojitenga mbali na kanisa. Papa alisema, imani si tu urithi wa utamaduni na mapokeo ya kijamii , lakini ni zawadi inayotolewa kwa mtu anayekutana na Yesu na ni uhuru na furaha kamili katika kuyakubali maisha mapya yaliyomo katika zawadi hiyo.

Papa pia aliita familia iliyo injilishwa , kuwa wakala wa thamani katika kueneza Injili. Na hivyo aliwahimiza Maaskofu wa Hispania, kuandaa vyema miito ya upadre. Na alimalizia hotuba yake kwa kusisitiza
upendo na huduma kwa maskini, kama ishara ya Ufalme wa Mungu , na Kanisa ni mama ambaye " hawezi kusahau watoto wengi wanao ishi katika hali ya kupungukiwa na mahitaji msingi ya binadamu








All the contents on this site are copyrighted ©.