2014-02-28 08:09:35

Waraka wa Injili ya Furaha uwe ni mwongozo wa tafakari ya Kwaresima 2014


Kardinali Agostino Vallini, Makamu Askofu Jimbo kuu la Roma, anawaalika Maparoko wote kufanya tafakari ya kina na hatimaye kuwashirikisha utajiri unaofumbatwa katika Waraka wa Kitume wa Baba Mtakatifu Francisko "Evangelii Gaudium", Injili ya Furaha katika kipindi cha Kwaresima kwa Mwaka 2014. RealAudioMP3

Kipindi hiki kinaanza kwa kupakwa majivu, alama ya toba na wongofu wa ndani, hapo tarehe 5 Machi 2014. Hayo yamo kwenye barua ambayo Kardinali Vallini amewaandikia Maparoko wa Jimbo kuu la Roma. Kwaresima kiwe ni kipindi cha kufanya tafakari ya kina kuhusu Waraka wa Kitume ulioandikwa na Baba Mtakatifu Francisko katika kufunga Mwaka wa Imani sanjari na kujikita katika Uinjilishaji Mpya.

Waraka huu una utajiri mkubwa wa kichungaji unagusa kwa namna ya pekee tema muhimu zinazopaswa kufanyiwa kazi katika mchakato wa Uinjilishaji Mpya. Waraka huu unaweza pia kuwa ni chimbuko la mipango na mikakati ya shughuli za kichungaji kwa Parokia mbali mbali Jimbo kuu la Roma kwa kujikita katika dhana ya Kanisa la Kimissionari, changamoto inayotolewa na Baba Mtakatifu Francisko katika Mapambazuko ya Millenia ya tatu ya Ukristo.








All the contents on this site are copyrighted ©.