Wito kwa ajili ya kuombea amani na utulivu nchini Venezuela
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya Katekesi yake, Jumatano tarehe 26 Februari
2014 anasema, anafuatilia kwa masikitiko makubwa yale yanayotendeka nchini Venezuela.
Anatoa wito kwa pande zote zinazohusika kuacha matumizi ya nguvu na uhasama
na kuanza mara moja kujikita katika mchakato wa upatanisho na msamaha wa kitaifa unaofumbatwa
katika majadiliano ya ukweli, kuheshimiana na haki kwa ajili ya mafao ya wengi.
Hizi
ni juhudi zinazopaswa kufanywa kwanza kabisa na wanasiasa pamoja na taasisi zinazohusika.
Baba Mtakatifu anapenda kuwahakikisha wote walioguswa na majanga haya uwepo wake wa
karibu kwa njia ya sala. Anawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema kuinua
sala zao kwa maombezi ya Bikira Maria kwa ajili ya kuombea amani na utulivu nchini
Venezuela.