Wahamiaji zaidi ya 300 wa Morocco , hivi karibuni walivamia uzio, wakijaribu kuvuka
mpaka kati ya Morocco na Hispania mkoani Melilla, maafisa wameripoti. Katika
harakati hizo, vikosi vya usalama vya Morocco , vilipambana na wahamiaji hao na
kusababisha watu 27 kujeruhiwa,na wengine tisini na sita wahamiaji walikamatwa, wakati
wengine 100 waliweza kuvuka mpaka. Wahamiaji wengi toka Afrika Kaskazini , hupenda
kuutumia mpaka huo ulio jangwani kuingia barani Ulaya kwa lengo la kutafuta kazi na
kuboresha maisha yao. Wengi wa hamajia hao ni tokea Eritrea na Somalia.
Idara
ya Mambo ya Ndani ya Hispania, imethibitisha uwepo wa kasheshe hilo la wahamiaji
, Ijumaa iliyopit, ambako polisi walilazimika kutumia risasi za mpira kuwazuia wahamaji
kuingia Hispania. Idara hiyo imekanusha risasi hizo kusababisha wahamiaji wengine
kuzama maji.