2014-02-24 08:25:35

Rais Rousseff wa Brazil akutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini Vatican


Baba Mtakatifu Francisko mwishoni mwa Juma amekutana na kuzungumza na Rais Dilma Rousseff wa Brazil na ujumbe wake waliokuwa mjini Vatican kushiriki katika Ibada ya kusimikwa kwa Makardinali wapya, kati yao alikuwepo Kardinali Oran Tempesta, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Rio de Janeiro, Brazil.

Baba Mtakatifu kwa mara nyingine tena ametumia fursa hii kwa ajili ya kuwashukuru wananchi wa Brazil kwa moyo wa ukarimu na upendo waliomwonesha wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2013 iliyofanyika nchini Brazil.

Kwa upande wake Rais Rousseff amemwelezea Baba Mtakatifu Francisko kuhusu maandalizi ya michezo ya Kombe la Dunia kwa Mwaka 2014 itakayofanyika nchini Brazil. Rais amemzawadia Baba Mtakatifu Francisko jezi ya mpira iliyotiwa mkwaju na "Mchawi wa Kabumbu" Pele kwa heshima ya Baba Mtakatifu Francisko pamoja na mpira uliotiwa sahihi na Ronaldo. Baba Mtakatifu kwa upande wake amemzawadia Rais Rousseff medali ya Malaika wa Amani.







All the contents on this site are copyrighted ©.