2014-02-24 14:56:15

Rais Michel Joseph Martelly wa Haiti akutana na kuzungumza na Papa Francisko


Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 24 Februari 2014 amekutana na kuzungumza na Rais Michel Joseph Martelly wa Haiti pamoja na ujumbe wake, ambao pia walikutana na kuzungumza na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu mkuu Dominique Mamberti, Katibu mkuu wa Mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.

Viongozi hawa wawili wameridhishwa na uhusiano kati ya Haiti na Vatican. Kwa pamoja wamepongeza mchango unaotolewa na Kanisa Katoliki nchini Haiti. Baba Mtakatifu ni mgeni wake wameonesha haja ya kuendelea kujifunga kibwebwe kwa ajili ya ujenzi wa Haiti mpya hasa kwa kuimarisha sekta ya elimu na afya pamoja na huduma za kijamii. Wamekazia pia umuhimu wa majadiliano ya amani kati ya makundi mbali mbali nchini Haiti ili kujenga upatanisho, umoja wa kitaifa na mafao ya wengi.







All the contents on this site are copyrighted ©.