Mzee Kenneth Kaunda, Muasisi wa Taifa la Zambia, Jumapili iliyopita alilazimika kulazwa
Hospitalini mjini Lusaka, Zambia kutokana na afya yake kuanza kudhoofu. Rais Michael
Sata wa Zambia amekwenda kumsalimia na kusema kwamba, hali yake inaendelea vyema kwa
sasa.
Itakumbukwa kwamba, Mzee Kaunda ana umri wa miaka 89 ni kati ya Marais
waliokuwa mstari wa mbele katika ukombozi, Kusini mwa Afrika.