2014-02-22 10:55:14

Papa kutangaza hadharani Makardinali wapya


(Vatican) Baba Mtakatifu Francisko , Jumamosi hii , ataongoza Mkutano wa Kawaida wa Makardinali wa hadhara , majira ya saa tano za asubuhi , katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, kwa nia ya kuwasimika Makardinali wapya 19, alio wateua hivi karibuni.
Maelezo yametolewa kwamba, kati ya makardinali hao wapya 16 wana umri chini ya miaka 80, na hivyo wana haki ya kupiga kura katika kikao cha Makardinali cha kumchagua Khalifa wa Mtume Petro kinacho julikana kama "Conclave", na pia haki ya kuchaguliwa kukalia kiti hicho. Watatu wana umri zaidi ya miaka 80 na hivyo hawana haki ya kuchagua au kuchaguliwa kuwa Papa.
Kati ya kazi muhimu za Baraza la Makardinali ni kumchagua Papa, lakini pia ni chombo cha ushauri cha kijadi ambacho kinaweza kuitwa kama "seneti ya Papa. Hivyo Papa Francisko pamoja na kuitisha mkutano wa Makardinali kwa nia ya kuwasimika Makardinali wapya, pia ameutumia uwepo wa Makardinali hapa Vatican, kujadili baadhi ya vipaumbele vinavyo hitaji marekebisho ya haraka . .
Ifuatayo ni orodha ya Makardinali wapya na historia yao fupi katika utumishi wa kanisa

Pietro PAROLIN
Tangu mwaka 1986, alikuwa akitumika katika Idara ya Diplomasia ya Jimbo la Papa, hadi mwaka 2009 alipo teuliwa kuwa mwakilishi wa Papa nchini Venezuela . Na mwaka 2013, Papa Francisko alimteua kuwa Katibu wa Jimbo Takatifu.

LORENZO BALDISSERI
Aliwahi kuwa Nuncio wa Papa Brazil. Na alifanywa kuwa Katibu wa Usharika wa Maaskofu Brazil, tangu January 2012 hadi alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa Sinodi ya Maaskofu iliyoitishwa na Papa Francisko Septemba 2013.

G erhard LUDWIG Muller
Mwaka 2012 aliteuliwa kuwa Mkuu wa Shirika kwa ajili ya Mafundisho Sadikifu ya Imani Katoliki, na pia Na Rais wa Tume ya Kanisa la Mungu , na Rais wa Tume ya Kipapa kwa ajili ya Biblia na Rais wa Tume ya Kimataifa ya Teolojia Ujeruman.

Beniamino STELLA
Amekuwa katika Idara ya Diplomasia ya Jimbo la Papa tangu mwaka 1970. Na hivi karibuni alikuwa ni Nunsio wa Papa nchini Cuba nai Colombia,hadi Septemba 2013, alipo teuliwa na Papa Francisko kuwa Mkuu wa shirika la ya Makreli Septemba 2013.


VINCENT GERARD NICHOLS
Hadi hivi karibuni alikuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki la England na Wales. Ameisha pia kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Birmingham ( Uingereza ) kati ya Mwaka 2000 Rangi 2009, na baadaye kuteuliwa kuwa Askofu Mkuu wa Westminster ( Uingereza ) .

LEOPOLDO Jose BRENES SOLÓRZANO
Aliteliwa na Papa Yohane Pauloo 11 kuwa Askofu Mkuu wa Managua (Nicaragua) hapo Machi 2005.

Gerald Cyprien LaCroix , I.S.P.X.
amekuwa ni sehemu ya uongozi katika Taassii ya Papa Pio X, tangu Mwaka 1975,akiwa Katibu Mkuu na Mkurugenzi Mkuuu wa taasisi hiyo , na pia Mkurugenzi Mkuu wa malezi ya kiroho wa jumuiya ya Uamusho mpya. Na aliteuliwa kuwa Askofu Mkuu wa Québec (Canada) na Papa Benedict XVI, Februari 2011.

Jean -Pierre Kutwa
Askofu Mkuu wa Gagnoa ( Ivory Coast) ,na tangu Mei 2006 aliteuliwa kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Abidjan ( Ivory Coast) Mei 2006.

ORANI Joao TEMPESTA , O. cist .
Aliteuliwa kuwa Askofu Mkuu wa São Sebastião Rio de Janeiro (Brazil) hapo Februari 2009

GUALTIERO BASSETTI
Awali alikuwa ni mjumbe wa Tume ya Maaskofu wa Italia kwa ajili ya Maisha ya Makreli na maisha yaliyowekwa wakfu. Na pia mi mjumbe katika Bodi Katoliki kwa ajili ya Utamaduni na Ushirikiano na makanisa ya Kiothodosi ya utamaduni wa Byzantine na Makanisa ya Mashariki ya Kiothodosi. Kwa Sasa ni Makamu wa Rais wa Mkutano Maaskofu Italia, na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Perugia - Città della Pieve (Italia) .

MARIO AURELIO PIOLI
Kwa Sasa ni Rais wa Tume ya Maaskofu kwa ajili ya Elimu Katoliki na Tume ya Maaskofu kwa ajili ya shughuli za Idara za Baraza la Maaskofu Katoliki Argentina. Pia aliteuliwa kuwa Askofu Mkuu wa Buenos Aires (Argentina) na Francisko Machi 2013.

ANDREW YEOM soo - JUNG
Askofu MKUU wa Seoul (Korea ya Kusini ) tangu Mei 2012. Awali kwa mfululizo alitumikia katika nafasi mbalimbali za juu katika utawala wa Parokia na seminari nchini Korea ya Kusini .

Riccardo EZZATI ANDRELLO , S.D.B.
Msalesiani, Awali alikuwa ni Askofu Mkuu wa MKUU wa Concepción (Chile) , na Desemba 2010 aliteuliwa kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Askofu MKUU wa Santiago (Chile) katika Desemba 2010.

Philippe NAKELLENTUBA Ouédraogo
Hapo Awali alikuwa mjumbe katika Shirika kwa ajili ya Uinjilishaji wa Watu, na kuteuliwa kuwa Askofu Mkuu wa Ouadraogo (Burkina Faso) na Papa Benedict XVI, Mei 2009.



ORLANDO Quevedo, O.M.I.
Mmisionari wa Oblates of Mary Immaculate, aliteuliwa Askofu wa Kwanza wa Kidapawan (Philippines) baada ya Jimbo jIpya kuundwa Novemba 1982, na baadaye kuteuliwa kuwa AskofuMkuu wa Jimbo Kuu la Cotabato (Philippines) mwaka 1998.

CHIBLY Langlois
Aliteuliwa kuwa Askofu wa Les Cayes (Haiti) Agosti 2011. Awali alikuwa ni Profesa katika masuala ya teolojia ya kichungaji katika semnari Kuu ya Mama Yetu ya Port- au -Prince (Haiti) na pia Profesa katika Taasisi ya Jimbo Katoliki ya Elimu Binadamu ya Jacmel (Haiti) .

LORIS Francesco Capovilla
Mwandishi wa habari , na mhariri wa Zamani wa gazeti la kila wiki la Venice ( Italia) , aliwahi pia kuwa Katibu wa Angelo Giuseppe RONCALLI , baadaye Papa John XXIII. Na likuwa Mjumbe wa Papa katika Madhabahu Mataktifu ya Loreto (Italia) tangu mwaka 1971 Hadi alipostaafu Mwaka 1988. Kwa sasa ana umri wa miaka 98, atakuwa ni Askofu Mkuu mzee wa tatu duniani na pia anakuwa ni mzee kuliko wote , katika decania ya Makardinali..

Sebastian AGUILAR , C.M.F.
Mmisionari wa Shirika la Moyo Safi wa Maria na awali alikuwa Askofu wa Leon ( Hispania ),na kwa sasa ni Askofu Mkuu mstaafu wa Jimbo la Pamplona ( Hispania ), ambalo aliliongoza tangu mwaka 1993 Hadi alipostaafu Mwaka 2007.

Kelvin EDWARD FELIX
Aliwahi kuwa Rais wa Baraza la Makanisa ya Caribbean, pia Mjumbe katika Baraza la Kipapa kwa ajili ya ajili ya Mazungumzo na dini zingine, na pia ni Askofu Mkuu Mstaafu wa Castries (Saint Lucia ) , ambako aliongoza Jimbo hilo tangu mwaka 1981 hadi alipostaafu Mwaka 2008







All the contents on this site are copyrighted ©.