Hotuba ya Katibu wa Vatican kwa kikao cha Consistori: alikuwepo pia Papa Mstaafu Benedikto
XV1.
Jumamosi hii , Ibada ya hadhara ya kikao cha kawaida cha Baraza la Makardinali, iliyo
fanyika kwa nia ya kuwataja na kuwasimika Makardinali wapya 19, iliyo fanyika ndani
ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro Vatican, Papa Msaatafu Benedikto XV1, pia likuwepo.
Papa Francisko kabla ya kuketi katika kiti chake alisalimiana na Papa Mstaafu
Benedikto kwa upendo mkuu ndani, udugu wa Kristu. Papa pia alipeleka salam zake za
matashi mema kwa Kardinali mpya Loris Francesco Capovilla, ambaye hakuweza kuhudhuria
kikao hiki kutokana na hali ya afya kuwa teke.
Kikao kilifunguliwa na hotuba
ya Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin, ambaye alikuwa ni mmoja wa Makardinali
waliosimikwa. Katika hotuba aliyoisoma kwa niaba ya Maaskofu na Makardinali wote,alitoa
slaam za dhati kwake yeye Papa Francisko, na kwa Papa Mstaafu Benedikto XV1, na kwa
pia alitoa salaam kwa Kardinali Loris Capovilla , ambaye hakuweza kuhudhuria tukio
hili.
Aliendelea kumshukuru Papa Francisko kwa imani kubwa iliyo ionyesha
kwao na wao wanatoa jibu lao kwa uaminifu, ukarimu na uvumilivu katika wito wao,
ulio fumbatwa katika ishara ya vazi jekundu kama ishara ya kutenda kwa ujasiri, hata
kama ni kupoteza maisha au kumwaga damu kwa ajili ya kuitetea Injili ya Kristu na
kanisa lake Takatifu la Mitume na katika kuwaongoza na kuongeza Imani ya Kikristo,
kwa amani na utulivu wa watu wa Mungu na kwa uhuru katika kulieneza Kanisa Takatifu
Katoliki la Ulimwengu.
Na kwamba, kama mwanzo wa safari yao katika wito
wa neema ya kuwa mfano bora kwa watu wote, wake kwa waume , ambao wamewasindikiza
kwa namna mbalimbali za maisha ,alisema Katibu wa Vatican kwamba , wamepata neema
ya kuelewa kwamba, kuwa mwanafunzi wa Yesu, ni kuugundua utakatifu na upendo , ambazo
ni fadhila zisizo kuwa na kipimo na inaweza pia kudai zawadi ya maisha - kama ilivyotokea
na inaendelea kutokea kwa Wakristo wengi katika dunia, na hivyo inakuwa ni jambo la
lazima kutangaza hadharani, kuridhia wito huu .
Na wanatambua kwamba, kuwa
Kardinali ni kuwa mjumbe na mhudumu wa kanisa hata wakati wa matatizo, vipingamizi
na vishawishi vingi, daima ni kuubeba msalaba na kufuata mfano wa Mwana wa Mungu ,
aliyekuja kukaa kati yetu kama mtumishi (cf. Lk 22: 0.25-27 ) . Ni kufuata nyayo
zake na kwa majitoleo binafsi kwa ajili ya upendo wake , na kwa unyenyekevu mkuu
kwa Kanisa bibi harusi wake, na juu ya Msalaba. '
Katibu wa Vatican, alieleza
na kurejea maneno ya Papa Mstaafu Benedict, kwamba, mbegu ya ngano iliyo shuka kutoka
kwa Baba hadi shamba la dunia , aiikufa kwa ajili ya kuleta matunda y amaridhiano.
Na hivyo , kuianza kazi hii mpya katika Chuo cha Makardinali, ina maana ya
kutenda vyema zaidi na kuwa wasaidizi wa Papa maalum , wakiwa katika umoja zaidi katika
Kanisa la Ulimwengu , katika huduma ya ukarimu, wema na mashahidi wa Umoja wa Kanisa
na katika mpanuko wake , unaofanikishwa na hamu mpya ya utendaji maalum wa kitume,
waliokabidhiwa kwao , na katika idara za Curia ya Roma na Makao makuu ya Mabaraza
ya Maaskofu mbalimbali.
Kardinali Mpya kwa niaba ya wenzake wote alikiri
ushirikiano, kutembea na kuishi pamoja chini ya maongozi ya Baba Mtakatifu Francisko
katika safari ya umoja wa uongofu wa kichungaji,na kitume, bila kuiachia hali ya
dunia kwenda kama inavyotaka, bali kufanikisha katika mikoa yote, utume wa kudumu
kwa mujibu wa mafundisho ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican ( Angalia EG 25).
Hotuba
ya Kardinali Parolin, ilimhakikishia Papa Francisko, maombi yao kwa Mama Maria, Mama
wa Mungu na Kanisa na Malkia wa Mitume. Pamoja na Mtakatifu Yosef, wenye Heri Yohane
Paulo II, na Yohane XXIII,na watakatifu wote kwa maombezi yao kwa ajili ya Baba
Mtakatifu , na kw ajili ya wote waliokuwa katika Ibada hii na Kanisa zima na dunia
kwa ujumla.