Siku ya tatu mkutano kwa ajili ya Baraza la Makardinali
(Vatican ) Padre Federico Lombardi, SJ , Mkurugenzi wa Ofisi ya habari ya Vatican,
Jumatano, alitoa Muhtasari kwa wanahabari juu ya Mkutano wa Baraza la Makardinali
8 ambao ulifanyika Jumanne mchana.
Padre Lombardi ameeleza kwamba, kuna waandishi
wa habari wengi wa kigeni walio wasili mjini Roma, kufuatilia mkutano wa Makardinali
wa “Consistori” utakao fanyika mwishoni mwa wiki . Na kwamba Jumanne alasiri, Mkutano
wa Makardinali Wanane , uliendelea na kazi yake, na ulipokea ripoti kutoka Tume
ya Rejea ya Shirika la Uchumi –MiundoTawala katika Kiti Kitakatifu ( COSEA ).
Padre
Lombardi alieleza kuwa, kutokana na matokeo ya taarifa hizo, Makardinali hao wanaandaa
mapendekezo yao watakayo yasilishwa kwa Baba Mtakatifu.
Aliendelea kuweka
bayana kwamba, mchakato huu hasa unalenga taasisi ya Vatican inayo husiana na
masuala ya uchumi na fedha, na Mashirika ya Katoliki ( IOR ) , inayojulikana kama
Benki ya Vatican. Na kwamba, ingawa Makardinali wameandika mapendekezo yao, kwa
mujibu wa tathmini yao wenyewe, mwenye kutoa maamuzi ya mwisho ni Papa mwenyewe.
Aidha Padre Lombardi alisema, mchana Jumatano , Makardinali 15 wajumbe wa Mkutano
wa Baraza la maandalizi ya Kikao cha Consistori tayari wamewasili Vatican kwa maandalizi
yao. Na kwamba wao pia watapokea ripoti za Tume mbili zilizotajwa hapo juu.