(Vatican )Katibu mkuu wa Vatican, Askofu Mkuu Pietro Parolin, ametoa wito wa kulinda
na kudumisha mapokeo ya liturujia na kufungua mlango wa neema ambayo yenye ina uwezo
wa kujipandikiza na kuhifadhi ukweli wake. Hili alilieleza katika homilia yake, wakati
wa Misa iliyo iongoza Jmanne asubuhi katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro. Ibada
hii ilikuwa ni sehemu ya Mkutano unaoendelea katika Kanisa kuu la Lateran , juu
ya Maendeleo ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican (Katiba ya Vatican II)toleo la mwaka
wa 1963, lillilo fanya mabadiliko makubwa katika Liturujia ya Kanisa.
Askofu
Mkuu Parolin amesema , Mtaguso huo ni "Hema" ambamo Mungu na mtu hukutana. Ni njia
iliyo daima wazi ambayo huleta Roho Mtakatifu kutoka mbinguni hadi duniani. Kwa miaka
elfu mbili, fikra za Kikristo zimepata maneno mengi kuelezea umuhimu wa Liturujia
ya Ekaristi. Na kwa miaka 51, ya Katiba ya Sacrosanctum Concilium, ni shara na kazi
inayowasilisha Uakatifu wa Mungu katika ubinadamu. Liturujia , amesema Askofu
Mkuu Parolin , inaruhusu utakaso wa mwanadamu kwa njia ya "ishara za neema katika
hatua ya kufanya nafasi mpya ,kwa ajili ya maisha ya ukombozi. Daima jambo hili
hushangaza, mara paleinapojidhihirisha katika hali ya unyenyekevu . Maisha ya Utatu
Mtakatifu tunaoupokea kupitia maji ya Ubatizo , Mungu anajitolea kama chakula katika
Ekaristi, na msamaha wake kwetu kwa njia ya ishara na maneno ya kikuhani :
Askofu
Mkuu Parolin alikamilisha homilia yake akisema, siri ya maisha ya Kristo , imemwilishwa
katika maisha ya kiroho ya Kanisa,na Liturujia inakuwa daima ni njia ya wazi na iliyojaa
maji safi ambayo hutoka katika chemchemi ya Pasaka ,siri ya Kristu. Liturujia hulinda
na kufungua mlango wa neema na huendelea kupandikiza na kutunza katika ukweli wake
na madhumuni yake ya kweli.