2014-02-19 11:28:59

Mahubiri ya Papa Francisko wakati wa Misa za asubuhi, yako mitaani!


Kitengo cha uchapaji cha Vatican, LEV, kimechapisha Kitabu cha Pili cha Mahubiri ya Baba Mtakatifu Francisko anayotoa kila siku wakati wa Maadhimisho ya Fumbo la Ekaristi Takatifu kwenye Kikanisa cha Mtakatifu Martha, kilichoko mjini Vatican. Hizi ni Ibada zinazohudhuriwa na makundi mbali mbali ya waamini kutoka ndani na nje ya Vatican.

Kitabu hiki cha Pili ni mkusanyiko wa Mahubiri ya Baba Mtakatifu Francisko kuanzia tarehe 2 Septemba 2013 hadi kufikia tarehe 31 Januari 2014. Kitabu hiki kwa sasa kinapatikana katika lugha ya Kiitalia na tafsiri yake kwa lugha ya Kiingereza iko mbioni kutolewa ili kutoa nafasi kwa waamini na watu wenye mapenzi mema kuendelea kufanya tafakari ya Neno la Mungu kadiri ya mawazo na changamoto inayotolewa na Baba Mtakatifu Francisko.

Kitabu hiki ni mfululizo wa Vitabu vingine sita vilivyoandikwa kuhusiana na mahubiri na hotuba za Baba Mtakatifu Francisko. Baadhi ya vitabu hivi ni "Maneno ya Papa Francisko" "Niombeeeni" "Usipokonywe matumaini", "Injili ya Furaha" Inapendeza sisi kuwepo hapa" "Mahubiri ya Papa Francisko" na "Tembeeni katika njia ya amani".







All the contents on this site are copyrighted ©.