Kardinali Ruini :waumini wapambana na mashinikizo ya kijamii na vikwazo
(Roma)Kardinali Camillo Ruini , Rais wa Shirika la Hija la Italia (Opera Romana Pellegrinaggi
(ORP) ) amesema katika miaka ya hivi karibuni waumini wanakiishi kishindo cha nguvu
za mashinikizo ya mazingira ya kijamii na kitamaduni , ambayo hutoa mtazamo kwamba,
maisha ya Kikristo ni kama vile yamepitwa na wakati wala si maisha endelevu.
Mashinikizo
yanayowafanya Wakristu kujisikia kama vile ni waathirika wa mambo ya kale yaliyopitwa
na wakati . Lakini Wakristu wanapaswa kuendelea na utambuzi wao kwamba imani haipitwi
na wakati, bali ni maisha endelevu yenye furaha kamili na nafasi ya kupumua anga
tofauti . Hayo yaliyaeleza siku ya Jumapili mjini Roma , katika hotuba yake ya uzinduzi
wa Mkutano wa Kazi za Kichungaji zha Teolojia kwa ajili ya ajili ya maadhimisho ya
80 ya hija Shirika la ORP . Kardinali Ruini alikuwa Rais wa Orp, tangu wakati akiwa
Vika wa Jimbo la Roma miaka ya nyuma.
Shirika la habari la SIR – limeripoti
kwamba, Kardinali alizungumzia haja ya kuwa na wakati na nafasi tofauti, kwa ajili
ya kupumua hewa tofuati kama vile kuwa na vipindi vya tafakari za kiroho na Hija
katika moja ya maeneo Matakatifu, kama ilivyo ilivyojionyesha katika uzoefu na
upembuzi yakinifu kwa watu wengi, hata miongoni mwa wale ambao huwa hawahudhurii Ibada
kanisani mara kwa mara. Na pia Hija, aliendelea – huweza kuwaweka pamoja vijana
na wazee na wengine wasiokuwa na mazoea ya kumcha Mungu .
Kardinali ametaja
kati ya siri ya hija iliyonzuri zaidi , ni upatikanaji wa viongozi wazuri si tu katika
kuzungumza na kuhubiri vizuri, lakini pia kusikiliza maoni ya wanahija kwa muda mrefu,
mbali na uwepo wa majadiliano katika makundi madogo madogo juu ya masuala ya kileo
na ya ushawishi wa mashinikizo ya jamii dhidi ya waamini leo .
Na aliongeza
kutafakari juu ya asili ya Hija, akibainisha kuwa , katika mchakato wa mapenzi kwa
malimwengu na ukana Mungu , unao ongeza pia kukua kwa wimbi jingine: la ubinafsi
wa kidini. Watu wengi wanaamini katika Mungu , na mara nyingi hata kwa Yesu Kristu,
na labda huomba, lakini wakipendelea kufanya hivyo kama mtu mwenyewe binafsi, bila
ya kujiunga na jumuiya yoyote ya Kikristu. Na sababu zinazotajwa na watu wa namna
hiyo, mara nyingi ni jeuri ya ubinafsi , wa mtu kutotaka kuingiliwa akiona kama anajitosheleza
mwenyewe, hivyo husema Yesu ndiyo, Kanisa
Katika mzamo huo, hija inaweza kuwa
tukio la kusaidia mtu wa namna hiyo, kugundua upya , furaha na nafasi ya mpya ktika
uzoefu wa maisha, manufaa ya kujumuika pamoja kama watu wa imani moja kutolea sala
na maombi , ambayo kiini chake ni mkusanyiko ndani ya Kanisa zaidi ya kuthamini
tu mikusanyiko ya pamoja katika masuala ya kidunia, nguvu ya kiuchumi, na kisiasa,
na hali halisi au bandia , ambayo daima hupendelewa na vyombo vya habari.
Kwa mujibu wa Kardinali Ruini, Hija ni fursa nzuri ya kujaribu kushinda na utengano
kizani au mbadala hewa, unaonekana mara kwa mara katika sala ya binafsi na sala ya
pamoja ya waamini. Ibada zinazofanyika wakti wa Hija amesisitiza , zinapaswa kukuza
umoja njia vizuri zaidi ya kuleta mwamko wa kuhudhuria pia ibada za Misa za siku
ya Jumapili , katika parokia.
Kardinali Ruini amekamilisha kwa kugusia mada
inayogusa katika mtima wa utamaduni wa leo ambamo watu kuwa na hisia za kutokuwa na
dhambi. Amesema hisia hizi ni kinagusa kiini asilia cha utamaduni na mawazo , ambayo
dhamiri au hisia ya dhambi inakuw ani ugonjwa wenye kuhitaji kuponywa na kujikwamua
. Kwa mujibu wa Kardinali, kugundua zaidi juu ya "hisia ya dhambi" inaweza kutokea
wakati wa Hija. Hija huwakilisha mwanzo wa njia mapya, ya maisha ya watu wengi ambao
pengine kwa muda mrefu wamekuwa mbali na Kanisa.