2014-02-18 11:10:06

Guinea kuendelea kupata msaada wa fedha kutoka IMF


Shirika la Fedha Duniani, IMF limeamua kuendelea kufadhili miradi mbali mbali ya maendeleo nchini Guinea iliyokuwa imebainishwa na Shirika hili mwaka mmoja uliopita. Licha ya hali ngumu ya kisiasa na kijamii, lakini bado wananchi wengi wa Guinea wanakabiliana na hali ngumu ya uchumi unaosababishwa na umaskini mkubwa kati ya wananchi wake.

Kuna baadhi ya wananchi wa Guinea wanaishi chini ya wastani wa dolla moja ya kimarekani kwa siku. Shirika la Fedha Duniani linaonesha kwamba, uchumi wa Guinea kwa Mwaka 2013 umekuwa kwa asilimia 2.5 kichume cha asilimia 4.5 kilichokuwa kimekadiriwa kwa Mwaka huo. Mfumuko wa bei ya bidhaa na huduma umepungua lakini bado ni wa kiwango cha juu. Shirika la Fedha Duniani limetoa kiasi cha dolla millioni 28. 2. Katika kipindi cha miaka mitatu, IFM itachangia kiasi cha dolla za kimarekani millioni 112. 8 za Kimarekani.







All the contents on this site are copyrighted ©.