2014-02-18 12:18:11

Boko haramu inaendelea kusababisha majanga nchini Nigeria


Askofu mkuu Ignatius Ayau Kaigama, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Nigeria anasema, mashumbulizi yaliyotokea nchini Nigeria hivi karibuni na kusababisha zaidi ya watu mia moja kupoteza maisha hayakuwashangaza kwani hii ni kampeni chafu inayofanywa na kikundi cha kigaidi cha Boko Haram kutaka kuwatisha na kuwajengea wananchi hofu isiyokuwa na msingi.

Askofu mkuu Kaigama anasema, inasikitisha kuona kwamba, Serikali na vyombo vya ulinzi na usalam bado havijafanikiwa kulinda na kutunza amani na utulivu wa wananchi wa Nigeria. Serikali imewekeza kiasi kikubwa cha rasilimali fedha na watu, lakini bado wananchi wasiokuwa na hatia wanaendelea kupoteza maisha yao kutokana na mashambulizi ya kigaidi.

Kuna haja kwa Nigeria kutafuta sababu msingi ili kuondokana na mashambulizi ya mara kwa mara yanayosababishwa na kiundi cha kigaidi cha Boko Haram nchini Nigeria. Inawezekana kwamba, kuna mtandao mkubwa wa kigaidi unaotekeleza lamelngo yake nje ya Nigeria anasema Askofu mkuu Ignatius Ayau Kaigama, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Nigeria.







All the contents on this site are copyrighted ©.