2014-02-17 15:08:16

Ziara ya nne ya Papa kutembelea Parokia Jimboni Roma.


Baba Mtakatifu Francisko , Jumapili iliyopita majira ya jioni alifanya ziara ya Kichungaji katika Parokia ya Mtakatifu Thomas Mtume iliyoko nje kidogo ya jiji la Roma, kwa nia ya kuvuvia na kuhamasisha uhusiano ukweli, uaminifu, na usafi wa moyo. Pia kutabaruki Kanisa Jipya katika eneo hilo. Kwa ajili hiyo, Papa aliongoza Ibada ya Misa iliyohudhuriwa na maelfu ya wakazi wa eneo hilo la Infernetto, Parokia ya Kusini mwa jiji la Roma ambayo ni sehemu ya Jimbo la Roma.

Papa katika Parokia hiyo alikaribishwa na umati mkubwa wa waaamini wakiongozwa na Kardinali Agostino Vallini , Vika wa Jimbo la Roma, akiwepo pia , Askofu msaidizi wa eneo hilo, Msgr Paolino Schiavon na Paroko Antonio D' Errico.

Akiwa katika Parokia hiyo, Papa alisalimiana na watoto na kuwapatia kile kilichiiotwa tiketi ya kuanza safari ya kutembea katika imani, akiwaambia siri ya kumpenda Yesu ni kumwachia yeye afanye kazi katika maisha yetu. Kwa kuwa Yeye alitupenda kwanza. Watoto hao wadogo wakiwa na nyuso za tabasamu waliinyosha mikono yao kwa Papa , huku wakisema, "Wewe ni rafiki yetu , na baadhi walipiga nae tano, Kisha alikutana na wazazi wa watoto waliobatizwa hivi karibuni wazee, wagonjwa , mapadre, na Chama cha Familia cha watoto wenye ulemavu. Na kabla ya Misa, alipata muda wa kuwaungamisha waaamini kadhaa.

Wakati wa Ibada , Papa aliangalisha homilia yake, katika somo la Injili , ambamo Mtakatifu Matayo anahimiza uhusiano mzuri kati ya mtu na mtu na hasa katika maeneo madogo ambamo watu hufahamiana kirahisi kwamba , ni lazima kuongozwa na misingi ya uaminifu na Ukweli . Ukweli unaotoka ndani ya moyo.

Papa aliwataka wote waliokuwa wamefika katika Ibada hyo, kila mmoja wao kuitafakari hali ya nafsi yake kama ni safi au chafu , ni kufikiri kilichomo ndani ya moyo na kuoana kama "Kuna upendo? Au kuna chuki ? Na iwapo kuna tabia ya msamaha kwa wale wanaotukosea na kutuumiza kimaisha au kuna tabia ya kulipa kisasi . Alikazia ni muhimu kujiuliza kilichomo ndani kwa sababu ndani ya hutoka yote matenda uovu, au wema . Na wema huupata uhuru moyo kuliko uovu.

Papa amekiri, ni kweli, kusamehe na kuwa mtu mwema si rahisi, lakini ni muhimu katika kuyatembea maisha matakatifu hasa katika kumpokea Bwana,na kuomba aingilie kati maisha yetu. Ni daima kuiomba neema hii ya kujua nini kinaendelea ndani ya moyo, na daima kufanya uchaguzi sahihi , uchaguzi wa mzuri. Ni kukumbuka kwamba matendo maovu katika maisha yetu huchafua roho zetu na kutuweka mbali na Bwana. Tuombe Bwana atusaidie daima, kuwa karibu nae, Papa alisisitiza. .

Hii ilikuw ani Parokia ya nne kutembelewa na Papa Francisko tangu kuanza utume wake mwaka jana. Mwishoni mwa Misa, Papa alitoa na shukrani kwa Paroko Padre Antonio d' Errico wa Parokia ya Mtakatifu Thomas Mtume, ambayo iko katika eneo lenye hili maarufu la Infernettalenye wakazi wapatao 25,000.








All the contents on this site are copyrighted ©.