Hivi karibuni, Mama Kanisa ameadhimisha Siku ya 22 ya Wagonjwa Duniani kwa kuitaka
Jumuiya ya Waamini kujenga na kuimarisha mshikamano wa upendo na wagonjwa.
Wagonjwa
nao wakakumbushwa kwamba, wanao mchango mkubwa katika maisha na utume wa Kanisa, kwani
wao bado ni sehemu ya Fumbo la Mwili wa Kristo, yaani Kanisa hata katika mahangaiko
na magonjwa yao!
Leo Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji
wa mitandao ya kijamii anawasihi wagonjwa wasikate tamaa hata wanapokabiliana na hali
ngumu ya magonjwa yao, bali waendeleee kuwa na matumaini, kwani Yesu Kristo daima
yuko karibu nao!