2014-02-17 11:12:56

Jeshi la kulinda amani la Umoja wa Mataifa litaendelea kuwepo nchini Burundi hadi Desemba 2014


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeamua kwamba, Vikosi vya Jeshi la kulinda amani la Umoja wa Mataifa vitaendelea kuwepo nchini Burundi hadi kufikia Mwezi Desemba 2014 kutokana na hali ya ulinzi na usalama kuanza kutetereka. Jeshi la Umoja wa Mataifa pamoja na mambo mengine limepewa dhamana ya kuhakikisha kwamba, mchakato wa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika nchini Burundi kunako mwaka 2015 unakwenda vyema. Hiki kitakuwa ni kipimo cha amani na utulivu kwa Burundi.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeridhika na hatua mbali mbali ambazo zimechukuliwa na Serikali ya Burundi katika kukabiliana na vikwazo vilivyojitokeza nchini humo mara baada ya vita ya wenyewe kwa wenyewe iliyosababisha majanga makubwa kwa watu na mali yao. Mabadiliko ya Katiba na tetesi za kutaka Rais Pierre Nkurunzinza aliyekuwepo madarakani tangu Mwaka 2005 kupewa tena nafasi ya kuiongoza Burundi kwa kipindi kingine cha awamu ya tatu, jambo ambalo ni kinyume cha Katiba ya Burundi.

Serikali ya Burundi inapinga wazo la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuendelea kuwepo nchini Burundi.







All the contents on this site are copyrighted ©.