Kumbukumbu ya Miaka 83 tangu kuanzishwa kwa Radio Vatican
Radio Vatican, Mama wa Radio zote duniani, tarehe 12 Februari 2014 imeadhimisha kumbu
kumbu ya Miaka 83 tangu ilipoanzishwa. Inajivunia kuwa ni kati ya wadau wakuu wa Shirikisho
la Watangazaji Barani Ulaya, EBU ambalo tarehe 13 Februari 2014 linaadhimisha Siku
ya Radio Duniani. Kwa namna ya pekee, Jumuiya ya Kimataifa kwa mwaka huu, inajielekeza
zaidi katika kuangalia mchango wa wanawake katika medani mbali mbali za maisha.
Watangazaji
wanawake kutoka Radio Vatican wamekuwa mstari wa mbele kwa kuwa ni sauti ya wanawake
wasiokuwa na sauti kutoka sehemu mbali mbali za dunia. Radio Vatican katika mtandao
wake imeandaa programe mbali mbali zinazoonesha mchango wa Radio Vatican katika kuwawezesha
wanawake Barani Afrika, Asia na Amerika.
Hizi ni programme zinazoonesha ujasiri
wa wanawake katika kukabiliana na changamoto mbali mbali za maisha: katika masuala
ya maendeleo endelevu, haki na amani duniani. Ukitaka kufaidi zaidi unaweza kutembelea
katika tovuti rasmi ya Radio Vatican kwa anuani ifuatayo: www.radiovaticana.va Unaweza
pia kuwashirikisha jirani zako.