2014-02-12 14:57:09

Vatican na Hungaria waridhia mkataba wa pamoja!


Tarehe 10 februari 2014, Vatican na Serikali ya Hungaria zimebadilishana hati za makubaliano kati ya nchi hizi mbili. Askofu mkuu Alberto Bottari de Castello, Balozi wa Vatican nchini Hungaria ameongoza ujumbe wa Vatican katika halfa hii. Kwa upande wa Serikali ya Hungaria, Dr. Zoltan Balog, Waziri wa rasilimali watu nchini Hungaria ameongoza ujumbe wa nchi yake.

Hati hizi zimefanya marekebisho ya msingi katika makubaliano yaliyokuwa yametiwa sahihi kati ya pande hizi mbili kunako tarehe 20 Juni 1997 kuhusu ruzuku ya fedha kwa huduma za kijamii zinaztolewa na Kanisa nchini Hungaria na mambo mengine yanayohusu urithi wa Kanisa nchini Hungaria, mkataba uliokuwa umetiwa sahihi tarehe 21 Oktoba 2013. baada ya kubadilishana hati za mkataba kadiri ya Ibara 7 ยง kifungu cha 2 mkataba huu umeanza kutekelezwa rasmi.







All the contents on this site are copyrighted ©.