Balozi Bassim awasilisha hati za utambulisho kwa Papa Francisko
Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi tarehe 6 Februari 2014 amepokea hati za utambulisho
kutoka kwa Bi Wafaa Ashraf Moharram Bassim, Balozi Mpya wa Misri mjini Vatican. Bi
Bassim alizaliwa kunako tarehe 21 Mei 1955 huko Heliopolis, ameolewa na ana watoto
watatu.
Balozi Bassim ana shahada ya uzamivu katika masuala ya kiuchumi. Tangu
mwaka 1978 amekuwa katika masuala ya kidplomasia kwenye Ubalozi wa Misri nchini Italia;
Mwakilishi wa Misri kwenye Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyoko mjini Geneva. Balozi,
Naibu Waziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa. Uongozi wa Vatican
unamtakia kheri na baraka Balozi Wafaa Ashraf Moharram Bassim katika dhamana na utume
wake mjini Vatican.