Watu 500 walipoteza maisha kutokana na vita ya kikabila nchini Kenya
Taarifa ya Umoja wa Mataifa inaonesha kwamba, katika kipindi cha Mwaka 2013 watu elfu
tano walipoteza maisha katika mapambano ya kikabila; kinzani kati ya wakulima na wafugaji
pamoja na uhasama wa kisiasa nchini Kenya. Kuna idadi kubwa ya wananchi waliojeruhiwa
na zaidi ya watu laki tano walilazimika kuyakimbia makazi yao.
Taarifa hii
imetolewa mapema juma hili na Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu misaada ya kibinadamu.
Idadi kubwa ya watu waliofariki dunia ni wale waliokumbwa katika mapigano yaliyotokea
Mwezi Desemba sehemu za Moyale, Mandera na kwenye Bonde la Mto Tana.