Injili inawachangamotisha waamini kujitosa kwa ajili ya jirani zao!
Ni tabia ya binadamu kujipenda na kujitafuta mwenyewe; kuponda mali na kusahau kwamba,
kuna maisha baada ya kifo. Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji
wa mitandao ya kijamii anasema, kwamba, ulimwengu na mazuri yake, yanawafanya watu
kujitafuta wenyewe; kuwa na mambo mengi pamoja na kufurahia maisha!
Baba Mtakatifu
Francisko anasema, Injili inawaalika na kuwachangamotisha waamini kujitoa katika ubinafsi
wao na kuwaendea jirani zao, ili kushirikisha na kuwaonjesa maskini na wote wanaosukumizwa
pembezoni yale waliyokirimiwa na Mwenyezi Mungu katika upendo wake.