2014-02-05 11:35:55

Mbinu mkakati wa kupambana na baa la njaa Ukanda wa Sahel


Shirika la Misaada ya Maendeleo la Watu wa Marekani, USAID katika kipindi cha miaka miwili, litachangia kiasi cha dolla za kimarekani millioni 130 kama sehemu ya mchakato wa kusaidia juhudi za Jumuiya ya Kimataifa kupambana na baa la njaa linalotokana na ukame wa muda mrefu kwenye Ukanda wa Sahel unaozijumuisha nchi za: Burkina Faso, Cameroon, Chad, Gambia, Mali, Mauritania, Niger, Nigeria pamoja na Senegal. Mchango huu utakuwa ni wa kipindi cha miaka mitano ili kushiriki kikamilifu katika maboresho ya maisha ya wananchi vijijini.

Kuna watu zaidi ya millioni ishirini wanaokabiliwa na baa la njaa Ukanda wa Sahel. Mtu mmoja kati ya kundi la watu nane ndiye mwenye uhakika wa usalama wa chakula kwenye nchi za Sahel. Serikali ya Marekani inapenda kuchangia katika mchakato wa maendeleo endelevu katika eneo la Sahel ambalo kwa sasa linakabiliana na majanga makuba kama vile: umaskini, ukosefu wa uhakika wa usalama wa chakula; ukame wa muda mrefu, vita pamoja na mashambulizi ya kigaidi.








All the contents on this site are copyrighted ©.