Urithi wa Mzee Madiba ni kiasi cha dolla za Kimarekani millioni 4.1
Hayati Mzee Nelson Mandela ameacha urithi wa dolla millioni 4.1 zitakazogawanywa kwa
mke wake Graca Machel ambaye ana haki ya kupata nusu ya urithi wote; sehemu ya mali
itagawanywa kwa wanafamilia, wafanyakazi, shule pamoja na Chama cha tawala cha ANC.
Hayo yamo kwenye wosia wa Mzee Mandela uliosomwa mahakamani, Jumatatu tarehe 3 Februari
2014.
Katika wosia huu, Winnie Madikizela- Mandela hakutajwa kati ya watu
wanaopaswa kufaidi na urithi ulioachwa na Mzee Madiba aliyefariki dunia tarehe 5 Desemba
2013 na kuzikwa siku 10 baaye kwenye Kijiji chake cha asili huko Qunu, baada ya wakuu
wa Jumuiya ya Kimataifa kutoa heshima zao za mwisho kwa Mzee Madiba ambaye baada ya
kushinda kinyang'anyiro cha Urais kunako mwaka 1994 alijikita katika siasa ya ukweli
na upatanisho, jambo ambalo lilimejengea sifa na heshima kubwa ndani na nje ya Bara
la Afrika.