2014-02-04 13:58:23

Malkia Elizabeth wa Uingereza kukutana na Papa Francisko tarehe 3 Aprili 2014


Baba Mtakatifu Francisko hapo tarehe 3 Aprili 2014 anatarajiwa kukutana na kuzungumza na Malkia Elizabeth wa Uingereza pamoja na ujumbe wake, ambao watakuwa mjini Roma kwa mwaliko wa Rais Giorgio Napolitano wa Italia. Malkia Elizabeth amealikwa na Serikali ya Italia kwa chakula cha mchana na baadaye atapata fursa ya kukutana na kuzungumza na Baba Mtakatifu Francisko.

Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Malkia Elizabeth kukutana na Baba Mtakatifu Francisko aliyechaguliwa kuongoza Kanisa Katoliki hapo tarehe 19 Machi 2013, baada ya Papa Benedikto XVI kung'atuka kutoka madarakani kwa hiyari yake mwenyewe. Kwa mara ya mwisho, Malkia Elizabeth wa Uingereza alitembelea mjini Roma tarehe 17 Oktoba 2000 wakati wa Maadhimisho ya Jubilee kuu ya Ukristo, akakutana na kuzungumza na Mwenyeheri Yohane Paulo II.

Malkia Elibeth alikutana na Baba Mtakatifu Benedikto XVI mwezi Septemba, 2010 wakati alipokuwa anatembelea Uingereza. Itakumbukwa kwamba, Malkia Elizabeth aliwahi kukutana na Papa Yohane XXIII kunako mwaka 1961. Habari hizi zimethibitishwa na Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.