Mama Kanisa kila Mwaka ifikapo tarehe 2 Februari anaadhimisha Siku ya Watawa Duniani
iliyoanzishwa na Mwenyeheri Yohane Paulo wa Pili kunako Mwaka 1997 kwa kuthamini mchango
wa maisha na utume unaotolewa na Watawa sehemu mbali mbali za dunia.
Baba
Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa Siku ya Watawa Duniani anawaalika Watu
wa Familia ya Mungu kutoa kipaumbele cha kwanza kwa Yesu katika maisha yao!