2014-02-02 09:21:45

Mshikamano wa upendo na kidugu kwa wananchi wa Ufilippini!


Askofu mkuu Joseph Kurtz, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani, kuanzia tarehe 2 hadi tarehe 7 Februari 2014 pamoja na ujumbe wake, watakuwa nchini Ufilippini, ili kutembelea maeneo yaliyoathirika vibaya kutokana na tufani iliyoikumbuka Ufilippini hapo tarehe 8 Novemba 2013 na hivyo kusababisha maafa makubwa kwa watu na mali zao.

Ziara hii ya upendo na mshikamano wa kidugu imeandaliwa na Shirika la Misaada la Kanisa Katoliki Marekani, ambalo limepokea kiasi cha dolla za Kimarekani millioni 50 kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wa Ufilippini waliokumbwa na tufani hii. Wakiwa nchini Ufilippini watapata nafasi ya kuzungumza na kutembelea Makanisa yaliyoathirika zaidi. Watakutana na kuzungumza na viongozi wa Kanisa nchini Ufilippini.

Changamoto ya kuwasaidia wananchi wa Ufilippini baada ya kukumbwa na maafa ilitolewa na Kardinali Timothy Dolan aliyekuwa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani, wazo ambalo lilifanyiwa kazi na matunda yake yanaonekana kwa sasa. Ni mchango kutoka kwa waamini na watu wenye mapenzi mema nchini Marekani.







All the contents on this site are copyrighted ©.