2014-01-30 08:49:09

Vatican na Malta watiliana sahihi mkataba kuhusu masuala ya ndoa!


Serikali ya Malta na Vatican, Jumatatu tarehe 27 Januari 2014, zimetiliana sahihi nyongeza katika mkataba uliokuwa umetiwa sahihi na pande hizi mbili kunako tarehe 3 Februari 1993 kwa kutambua kisheria ndoa zinazofungwa ndani ya Kanisa na Maamuzi ya Mahakama za Kanisa kuhusu ndoa.

Askofu mkuu Aldo Cavalli, Balozi wa Vatican nchini Malta ameuwakilisha ujumbe wa Vatican katika tukio hili na serikali ya Malta imewakilishwa na Bwana Owen Bonnici, Katibu wa Bunge katika masuala ya haki. Protokali hii ina Ibara kuu nne zinazofanya mabadiliko katika Mkataba uliotiwa sahihi kunako Mwaka 1993.







All the contents on this site are copyrighted ©.