Watu 26 wafariki dunia baada ya Kanisa kushambuliwa nchini Nigeria
Kikundi cha Boko Haram, jumapili iliyopita, tarehe 26 Januari 2014 kimefanya shambulizi
katika Kanisa Katoliki, Kaskazini mwa Nigeria na kusababisha vifo vya watu 26. Boko
Haram pia ilifanya mashambulizi kwenye baadhi ya nyumba zilizoko karibu na Kanisa.
Viongozi
wa Kanisa na Serikali wamekiri kutokea kwa shambulio hili linaloendelea kujenga hofu
na wasi wasi miongoni mwa wananchi wa Nigeria, wanaopaswa kushikamana katika umoja
na udugu na kutokubali kutumiwa na baadhi ya watu wanaotaka kujinufaisha wenyewe kutokana
na migogoro ya kidini.
Itakumbukwa kwamba, kunako tarehe 26 Januari 2014 Kikundi
cha Boko Haram kilivamia Vijiji vya Kauwuri na Wala na kusababisha vifo vya watu 54.