Jitahidini kuuishi Ubatizo wenu kila siku, kwa kumvaa Kristo!
Wakati huu Wakristo wanapojiandaa kufunga rasmi Juma la Kuombea Umoja wa Wakristo
sanjari na Siku kuu ya Kuongoka kwa Mtakatifu Paulo, mwalimu na mtume wa Mataifa,
hapo tarehe 25 Januari 2014.
Baba Mtakatifu Francisko anawakumbusha waamini
kwamba, wanashikamanishwa na Kristo kwa njia ya Ubatizo na Fumbo la Msalaba. Katika
ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii, Baba mtakatifu anawaalika waamini
kuhakikisha kwamba, wanaishi Ubatizo wao kila siku, wakijitahidi kuwa ni viumbe wapya
waliozaliwa kwa Maji na Roho Mtakatifu, kiasi cha kumvaa Kristo na kuanza kutembea
katika mwanga wa maisha na utu mpya!.