2014-01-23 08:51:57

Ombi la Papa kwa ajili ya amani ya Syria


Jumatano, Papa Francisko mara baada ya kukamilisha Katekesi yake kwa mahujaji na wageni, aliwaombea viongozi wanaokutana Geneva Uswiss kwa ajili ya kuzungumzia majawabu yanayoweza kumaliza vita ya Syria. Vita hii ya Syria, imesababisha zaidi ya watu 100 elfu kupoteza maisha na mamillioni wengine kuishi ugenini kama wakimbizi.
Mkutano huu unaojulikana kama Geneva II , ni mkutano wa kimataifa kwa ajili ya amani nchini Syria, ulifunguliwa Jumatano, Januari 22 , mjini Montreaux , Uswisi na majadiliano yanaendelea Geneva hadi Ijumaa, Januari 24, na unahudhuriwa na viongozi wa kisiasa, kidini na wataalam wa sera. Akizungumza mwishoni mwa Katekesi yake, Papa Francisko alimwomba Bwana aiguse mioyo ya watu wote wanaohusika katika mgogoro huu na pia washiriki wa mkutano wa Geneva II , ili waweze kutazama tu yaliyo mema kwa watu wa Syria hasa kwa wakati huu wa majaribu makubwa kwa Wasyria , ili waweze mara moja kukomesha vurugu na kufikisha mwisho wa vita , ambayo tayari inasababisha mateso makubwa hasa wka watu wasiokuwa na hatia au uwezo wa kujitetea.

Baba Mtakatifu Francisko alionyesha tumaini lake kwamba , taifa pendwa la Syria, litapendelea kutembea tena katika njia ya amani, maridhiano , na ukarabati unaowashirikisha raia wote wa Syria , ili kwamba kila mmoja aweza kumwona mwingine kuwa si adui , au mpinzani, lakini kama ndugu kuwakaribishwa na kukumbatiwa.
Utume wa Bahari
Aidha Papa aliutumia muda huo wa kutoa katekesi kwa mahujaji na wageni, pia kutoa salaam zake maalum na kuwakaribisha kwa Waratibu wa Kimkoa wa Utume wa Kichungaji katika ulimwengu wa Bahari, wanaokutana Rome wiki hii. Katika hotuba yake fupi , Papa Francisko alitoa wito kwa wale wanaofanya kazi kwa ajili ya ustawi wa mabaharia na familia zao , kuwa sauti ya wale wanaoishi mbali na wapendwa wao na wale wanao pambana na hali hatarishi na gumu, katika kazi yao baharini.

Mkutano katika Rome , unafanyika chini ya udhamini wa Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya kazi za Kichungaji kwa Wahamiaji na watu wasiokuwa na makazi maalum , Kardinali Antonio Maria VegliĆ² . Mkutano huu wa Wakurugenzi wa Mkoa unajadili changamoto zinazo kabili Utume wa Kichungaji katika Mkoa wa Bahari.








All the contents on this site are copyrighted ©.