Ujumbe wa Papa Francisko kwa kongamano la kiuchumi- Davos
Baba Mtakatifu Francisko akijali kila hali ya maisha ya watu duniani, alituma ujumbe
wake kwa washiriki wa Kongamano la Kiuchumi la Duniani, lililofunguliwa katika mji
wa mapumziko wa Davos Uswiss, jioni ya Jumanne 21 Januari 2014. Ujumbe wa Papa ulitumwa
kwa Profesa Klaus Schwab, Mwenyekiti Mtendaji wa Kongamnao la Uchumi Duniani.
Viongozi
wa Kanisa Katoliki ni miongoni mwa wale wanaoshiriki katika kongamano hili la siku
nne , ambalo linaongozwa na kauli mbiu ” Mfumo mpya wa dunia : Matokeo yake kwa
jamii, Siasa na Biashara. Katika ujumbe huu, Papa Francisko anasema ni muhimu kusifu
hatua zinazochukuliwa kwa lengo la kuboresha hali ya maisha ya watu katika maeneo
ya afya, elimu na mawasiliano na kutambua jukumu la msingi kwamba, utendaji wa sasa
katika biashara unatakiwa kuleta mabadiliko chanya.
Hata hivyo, anasema,
baadhi ya mafanikio yaliyopatikana, kwa bahati mbaya, yameongeza kusababisha kuenea
kwa jamii kutengana, na hasa mpanuko wa pengo, kati ya maskini na matajiri, waume
kwa wake ambao bado wanateswa na madhara ya ukosefu wa usalama kila siku.
Papa
Francisko amesisitiza, jukumu muhimu kwa wanasiasa na wachumi, ni kukuza mbinu za
utendaji zenye kujenga ushirikiano na umoja, ambamo utu wa kila binadamu na manufaa
ya wote huzingatiwa. Anasema suala hili, ni lazima liwe msingi wa kufanya maamuzi
ya kila mfumo wa kisiasa na kiuchumi, ambalo mara nyingi hupewa uzito kidogo. Papa
ameeleza na kukumbusha pia kwamba, wale wanaofanya kazi katika sekta hizi, wana wajibu
nyeti kwa maisha ya wengine, hasa watu dhaifu zaidi na wanaoishi katika mazingira
magumu.
Papa anasema, kwa watu wenye mapenzi mema, ni ngumu kuvumilia kuona
kwamba, maelfu ya watu wanaendelea kufariki dunia kila siku kutokana na njaa , ingawa
dunia ina chakula cha kutosha ambacho huharibika bure. Na pia si rahisi kuacha kujali
hali ya wakimbizi wanaotafuta kuboresha maisha yao, hasa wale wanaopambanishwa na
hali ngumu katika nchi mpya wanazo ingia wale wanao ishia kuangamia.
Papa
Francisko amemalizia ujumbe wake kwa kutaja kinachohitajika kwa sasa , ni uwepo
wa mwono mpya, uwazi na kupanua zaidi hisia za uwajibikaji kwa wahusika wote, unaoweza
kuongoza shughuli za kiuchumi na fedha kwa uadilifu na utu zaidi.