2014-01-22 11:16:09

Mshikamano wa dhati na wananchi wa Sudan ya Kusini


Baraza la Maaskofu Katoliki Sudan Kongwe na Sudan ya Kusini, Jumanne tarehe 21 Januari 2014 limeanza mkutano wake wa dharura unaotarajiwa kukamilishwa hapo tarehe 30 Januari 2014 kwa kutoa tamko rasmi la Baraza la Maaskofu Katoliki Sudan kuhusu kinzani na vita inayoendelea nchini Sudan ya Kusini.

Mkutano wa Maaskofu unafanyika wakati muafaka ambapo wananchi wa Sudan Kongwe na Sudan ya Kusini wanakabiliana na hali ngumu ya maisha kutokana na vita na kinzani za kijamii zinazoendelea kusababisha maafa makubwa kwa watu na mali zao.

Baadhi ya hati za kusafiria za viongozi wa Kanisa kutoka Sudan kongwe zinashikiliwa na vikosi vya ulinzi na usalama kiasi kwamba, wameshindwa kuhudhuria mkutano wa Baraza la Maaskofu Katoliki Sudan Kongwe na Sudan ya Kusini.

Safari ya kikazi iliyofanywa na Askofu mkuu Charles Daniel Balvo Balozi wa Vatican nchini Sudan ya Kusini imeonesha moyo wa mshikamano na wananchi wa Sudan ya Kusini kutoka kwa Mwakilishi wa Baba Mtakatifu.

Licha ya majanga yanayoendelea kujitokeza Sudan ya Kusini, lakini bado waamini wanaendelea kuishuhudia imani yao kwa ujasiri, furaha pamoja na mshikamano kwa njia ya sala.







All the contents on this site are copyrighted ©.