Kardinali ahimiza Wanasiasa Sudan Kusini kujenga amani na maridhiano
Askofu Mkuu Zuberi Kardinali Gabriel Wako wa Jimbo Kuu la Khartoum Sudan , ametoa
ombi kwa viongozi wa kisiasa, Sudan Kusini, kuweka kando maslahi yao binafsi, wanapotafuta
ufumbuzi wa mgogoro wa kisiasa katika taifa lao changa la Sudan Kusini. Kardinali
Wako , alieleza hilo akiwa Juba, Mji Mkuu wa Sudan ya Kusini,ambako ana hudhuria
Mkutano wa Baraza la Maaskofu Katoliki wa Sudan na Sudan Kusini. Ametoa wito kwa
Sudan Kusini kutambua kwamba , binadamu wote ni wana wa Mungu , na hivyo kuu ni dhambi.
Mapambano kati ya viongozi waweili pinzani katika chama tawala cha SPLM ( Sudan
Watu Liberation Movement ), Rais Salva Kiir na aliyekuwa Makamu wa Rais Riek Machar,
kwa sasa yanaonekana kuwa na mwelekeo wa mgawanyiko wa kikabila, makabila mawili
makubwa nchini Sudan Kusini, Wadinka na Wanuer .
Wakati huo huo, licha ya mazungumzo
yanayoendelea Addis Ababa Ethiopia kati ya wawakilishi wa wapinzani hao wawili ,
vita inaendelea, hasa katika eneo la mji wa Malakal , Mji muu wa Jimbo la Upper Nile,
( kaskazini-mashariki ). Hapo Januari 18, jeshi liliweza kuchukua udhibiti wa Mji
wa Bor , ambao ni Mji Mkuu wa Mkoa wa Jonglei (Mashariki). Mapigano haya hasa yanafanyika
kAtika mikoa yenye utajiri mkubwa wa rasIlimali. Mapambano yalianza Desemba 15.
Mkoa mwingine ulio katika vita hivi ni Mkoa wa UNITA ambao mji wake Mkuu ni Bentiu
.
Kuna hofu kwamba, iwapo mapigano hayatasitishwa hivi karibuni, Sudan Kusini
itazama katika dibwi la umwangaji wa damu na uharibifu wa kivita, utakaolazimu pia
vikundi vingine vyenye silaha na kuvikundi vingine vya kikabilia kuingilia kati na
hivyo kuwa ni maafa yasiyo elezeka. Mpaka sasa machafuko yanayoendelea yameingia
katika mwelekeo wa kimataifa , baada ya jeshi la Uganda kujiunga na jeshi la Kiir
wakati pia Kenya imepeleka kikosi chake kwa ajili ya kulinda raia wake wanaioshi na
kufanya kazi Sudan kusini, Shirika la habari la Fides limetaarifu. .