2014-01-21 08:48:21

Jifunueni wazi kwa Injili na maajabu ya Mungu – Papa Francisko


Jumatatu , Baba Mtakatifu Francisko, alisema uhuru wa Mkristo hupatikana katika utulivu wa kulisikiliza Neno la Mungu na kuliishi. Papa alieleza wakati akihubiri katika Ibada ya Misa, asubuhi, katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta, ndani ya Vatican. Papa alisema daima ni lazima kuwa tayari kuupokea ujumbe wa injili na miujiza ya Mungu aliyo ihifadhi kwa ajili yetu sisi.

Alisisitiza kwamba, Neno la Mungu ni hai, lina nguvu kamili , na hutambua hisia za moyo , lakini katika kulipokea, kwanza ni lazima kulipenda na kuwa tayari kulipokea kwa moyo wazi. Katika Mahubiri hayo, Papa alionyesha umuhimu na haja ya kweli, katika kuupokea ujumbe wa injili kwamba, inahitaji kujenga tabia ya usikivu na uwazi.

Na aliweka bayana kwamba, Injili si , tu , hutuambia yale tunayotaka sisi kusikia, lakini ni hai na lina nguvu na ni kamili. Neno la Mungu - aliendelea – hutolewa bila gharama yoyote, ni kamili na limejaa mambo mengi ya kustajaabisha,kwa sababu Mungu wetu ni Mungu wa Maajabu , Mungu wa Ufunuo.

Neno hili linatuhimiza kubadilika na kuwa watulivu.Lakini ni muhimu kwanza kupata ufahamu wa kina , nini maana ya kujiingiza katika mambo mapya ya injili. Na alionya dhidi ya kuwa wadadisi wa kupita kiasi, watu wa kupenda kuuuchakachua ujumbe wa Injili hadi kuwa jambo tofauti na lengo la Mungu.

Papa Francisko alileleza hayo akirejea masomo ya siku ya Jumatatu , ambamo Nabii Samweli, anamkaripia Mfalme Sauli kwa kutotii sauti ya Bwana na kwa kujaribu kuhalalisha uasi wake kwa kuufunika ulafi wake kwa ukarimu. Papa alisema ni muhimu kuwa na tulivu na moyo mtiifu ,wenye kusikiliza sauti ya Bwana, na kufanya kile anachoamuru, ili katika kumtii, inakuwa ni kushiriki katika maisha na upendo wake.

Na hii aliendelea, linatuongoza sisi katika kutafakari juu ya uhuru wa kweli wa Mkristu na maana ya utii wa Mkristu, ambavyo vyote viwili , hupatikana katika neno la Mungu na katika ujasiri wa kweli , wa kuwa wazi katika ujumbe wake.

Jumatatu , Baba Mtakatifu Francisko, alisema uhuru wa Mkristo hupatikana katika utulivu wa kulisikiliza Neno la Mungu na kuliishi. Papa alieleza wakati wa homilia yake ya Ibada ya Misa, asubuhi, katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta, ndani ya Vatican. Papa alisema daima ni lazima kuwa tayari kuupokea ujumbe wa injili na miujiza yake aliyo ihifadhi kwa ajili yetu sisi.

Alisisitiza kwamba, Neno la Mungu ni hai na huwa na nguvu kamili , na hutambua hisia za moyo , lakini kwanza ni lazima kuwa wazi katika kulipokea. Akiwahutubia walioshiriki katika Ibada hiyo ya Misa, Papa yalionyesha umuhimu na haja ya kweli, katika kuupokea ujumbe wa injili, katika kujenga tabia ya usikivu na uwazi.

Papa aliweka bayana kwamba, Injili - si tu hutuambia yale tunayotaka sisi kusikia, lakini ni hai na lina nguvu na ni kamili. Neno la Mungu - aliendelea – hutolewa bila gharama yoyote, ni kamili na limejaa mambo mengi ya kustajaabisha,kwa sababu Mungu wetu ni Mungu wa Maajabu , Mungu wa Ufunuo.

Neno hili linatuhimiza kubadilika na kuwa watulivu. Na ni muhimu kwanza kupata ufahamu wa kina nini maana ya kujiingiza katika mambo mapya ya injili. Na alionya dhidi ya kuwa wadadisi wa kupita kiasi, watu tunaopenda kuuuchakachua ujumbe wa Injili hadi kuwa jambo tofauti na lengo la Mungu.

Papa Francisko alileleza hayo akiarejea masomo ya siku ya Jumatatu , ambamo Nabii Samweli, anamkaripia Mfalme Sauli kwa kutotii sauti ya Bwana na kwa kujaribu kuhalalisha uasi wake kwa kuufunika ulafi wake kwa ukarimu. Papa alisema ni muhimu ni kuwa na tulivu na moyo mtiifu , kusikiliza sauti ya Bwana, na kufanya kile anacho tuamrisha kufanya ili katika kumtii, inakuwa ni kushiriki katika maisha na upendo wake.
Na hii aliendelea, inatuongoza sisi katika kutafakari juu ya uhuru wa kweli wa Mkristu na maana ya utii wa Mkristu, vyote viwili , hupatikana katika neno la Mungu na katika ujasiri wa kweli wa kuwa wazi katika ujumbe wake.








All the contents on this site are copyrighted ©.