2014-01-20 09:04:46

Wakristu toeni cheche za imani yenu kila siku.


Jumapili, Papa Francisko alifanya ziara ya Kichungaji , katika Kanisa la Moyo Mtakatifu wa Yesu la Roma , katika mtazamo wa adhimisho la 100 tangu Kanisa kuanzisha Siku ya Kimataifa kwa ajili ya kujali hali ya Wahamiaji na Wakimbizi.
Kanisa hilo, ambalo pia lina hadhi ya Basilika, lililoko karibu na Kituo cha Kikuu Treni cha Kati, jijini Roma , huendeshwa na Wamisionari WaSalesians ya Don Bosco, ambao huhudumia kwa ukarimu wageni wanaoingia jijini Roma bila kuwa na makazi. Kituo hicho kina uwezo wa kuhudumia hasa vijana wakimbizi wanapatao 400 wanaotaufuta hifadhi kutoka maeneo yenye ghasia za mapigano ya kisiasa kama Somalia , Eritrea , Gambia, Cameroon, Ghana , Congo , Ivory Coast, Afganistan , Iraq, Iran, Kurdistan, Misri , Syria , Sudan, Pakistan na Uturuki .

Akiwa mahali hapo , Papa Francisko alitoa wito kwa Wakristo katika kila hali ya maisha - na hasa watawa, kuionyesha dhahiri imani yao ya upendo wa injili ambao ni kujali na kutoa msaada kwa wahitaji kama kipaumbele cha kwanza katika kazi zao na katika kuishuhudia Injili kwenye maisha yao ya kawaida ya kila siku. Kati ya huduma zinazotolewa katika Kanisa hili la Moyo Mtakatifu ni pamoja kujifunza Kiitaliani, masomo ya Udreva wa magari , elimu ya msingi , elimu ya kompyuta mafunzo ya kazi na mipango.

Ziara hii ya iliyochukua takribani muda wa saa nne , Papa alikutana watoto na waamini wa Parokia katika ukumbi wa Basilica, kufanya mkutano na wakimbizi, na pia kukutana na watu wasio na makazi , kubadilishana salamu na familia ambazo zilikuwa na watoto walio batizwa kipindi cha mwaka uliopita , na pia wenyeji wake katika Kanisa hilo, jumuiya Wasalesiani na vijana na hatimaye kuongoza Ibada ya Misa.









All the contents on this site are copyrighted ©.