2014-01-20 15:14:19

Papa Francisko akutana na Mtawa Arturo, mkongwe wa miaka 101.


Siku ya Jumamosi jioni , Papa akiwa katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta, alimpokea ,mtawa Arturo Paoli, Mzee mwenye umri wa miaka 101, na kuwa na mazungumzo ya faraghani.
Inaelezwa Papa katika mazungumzo na Mtawa huyo wa Shirika la Ndugu wadogo wa Yesu, walizumgumzia zaidi kazi zake katika maisha ya kidini na kijamii kwa ajili ya watu maskini, nchini Italia na Amerika ya Kusini, ambapo ameitumia miaka 45 ya maisha yake.
Mtawa Arturo Paoli, kwa sasa anaishi katika nyumba ndogo ya Mtakatifu Charles de Foucauld , iliyoko karibu na mji wa wake wa kuzaliwa wa Lucca . Wiki chache zilizopita Paulo alionyesha waziwazi nia ya kutaka kukutana na Papa Francisko , na hivyo kukafanyika mpango kwa mkongwe , aweze kukutana na Papa. Na walikutana na kuwa na mazunguzo kwa takrbani dakika 40 katika hali ya utulivu na faragha.

Mkongwe Paoli aliishi Amerika ya Kusini, Argentina kwa miaka 14 , tangu 1960 mpaka 1974, ambako alikutana Padre Jorge Bergoglio, wakati ule akiwa Mkuu wa kanda kwa WaJesuits . Kisha aliondoka Argentina, hadi Venezuela na kuhamishiwa Brazil 1985 katika Brazil hadi kurejea Italia mwaka 2005.








All the contents on this site are copyrighted ©.