2014-01-20 10:02:04

Msipoteze matumaini katika uwepo wa dunia bora zaidi-Papa Francisko.


Jumapili , Baba Mtakatifu Francisko wakati wa sala ya Malaika wa Bwana, katika kuiadhimisha Siku ya Kanisa ya Wakimbizi na wahamiaji , alitoa himizo kwa wakimbizi kutopoteza matumaini ya kuingia tena katika dunia bora zaidi . Aidha alitoa shukurani zake za dhati kwa wote wanaojitolea kutetea ubinadamu.

Adhimisho la Siku ya Kanisa ya Kimataifa kwa ajili ya Wakimbizi Duniani, huadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Januari. Kwa mwaka huu imeongozwa na Mada Mbiu: "Kuelekea Dunia Bora Zaidi". Hotuba ya Papa alilenga katika kuwajali wanaoishi kwenye mazingira magumu akisema, upendo ni njia pekee ya kushinda uovu na dhambi.
Katika maelezo yake, mbele ya melfu ya mahujaji na wageni waliokuwa wamekusanyika katika uwanja wa kanisa kuu la Mtakatifu Petro, alirejea maneno ya Mwinjilishi Yohane Mbatazaji “Tazama Mwana-kondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu"akisema , Yohana Mbatizaji, anatambua Yesu alikuja duniani kwa kazi moja tu , nayo ni kumweka mtu huru dhidi ya utumwa wa dhambi, na alitoa malipo ya kifo cha msalabani, kumkomboa binadamu kutoka dhambi zake.

Kwa namna gani? Kwa njia ya Upendo. Hakuna njia nyingine ya kuondokana na uovu na dhambi , lakini kwa upendo unaoongoza katika kuipokea zawadi ya maisha ya majitolea kwa ajili ya wengine. Hivyo Yesu , alibeba mateso yetu na maumivu yetu, kwa gharama ya kifo chake juu ya msalaba.

Yeye ni kweli Kondoo wa Pasaka, aliyezama katika kilindi cha dhambi zetu, na kututakatifusha. Mtu na Mungu kweli, aliye jipanga katika mstari wa wenye dhambi ili abatizwe, ingawa hakuhitaji kufanya hivo. Lakini alifanya hivyo ili kuudhihirishIa ulimwengu kwamba ni Mtu aliyetumwa na Mungu Baba ulimwenguni kama kondoo wa dhabihu.

Papa alieleza leo hii inamaanisha nini kuwa wanafunzi wa Yesu, Mwana-kondoo wa Mungu ,akisema kwamba ni kuuweka ubaya na dhambi kando kwa kutumia nguvu upendo na unyenyekevu badala ya kiburi. Na badala ya majivuno ni kuhudumia.

Papa alisisitiza , msikubali kubaki na ufahali wa mahekalu bandia yaliyojengwa katika vilele vya mlima, lakini kuweni watu wapole na walio wazi katika kukaribisha na kupokea wengine hasa wenye shida kama wakimbizi na wahamiaji.

Na baada ya sala ya Malaika wa Bwana, Papa kwa namna yakipekee alipeleka salaam zake za mataishi mema kwa wawakilishi wa jamii na makabila mbalimbali waliokuwa wamekusanyika katika uwanja huo wa Mtakatifu Petro . Na aliwahakikishi kwamba, wako katika moyo wa Kanisa kwa sababu Kanisa ni watu walio katika safari kuelekea Ufalme wa Mungu, ulioletwa na Yesu Kristu kati yetu.

Mapema, Papa aliotoa Ujumbe kwa ajili ya adhimisho la mwaka huu 2014 , unaongozwa na MaNdhari “ Wahamiaji na Wakimbizi kuelekea dunia bora zaidii, uliochapishwa Agosti ya mwaka 2013. Katika ujumbe huo , ameaandika, mabadiliko ya tabia kwa wahamiaji na wakimbizi yanahotaji kila mtu, kujiweka mbali na mitazamo ya upinzani na hofu na aina zote za utamaduni wa kubaguana na kuelekea katika mitazamo msingi juu ya utamaduni wa kukutana , utamaduni wenye uwezo wa kujenga maisha bora zaidi, kwa haki na udugu.








All the contents on this site are copyrighted ©.