Baba Mtakatifu Francisko anaunga mkono maandamano yanayofanyika nchini Ufaransa kwa
ajili ya kulinda na kutetea Injili ya Uhai. Hayo yamebainishwa na Askofu mkuu Luigi
Ventura, Balozi wa Vatican nchini Ufaransa ambaye amemwelezea kwa kina na mapana juhudi
za Kanisa pamoja na watu wenye mapenzi mema kutaka kuenzi tunu msingi za maisha ya
ndoa na familia, dhidi ya utamaduni wa kifo unaokumbatia sera za utaoji mimba na hali
ya kutojali mateso na mahangaiko ya wengine.
Baba Mtakatifu anawaalika Waamini
na watu wote wenye mapenzi mema, kukumbatia na kuenzi Injili ya Uhai. Changamoto hii
pia imetolewa na Baba Mtakatifu Francisko, hivi karibuni alipokutana na kuzungumza
na Mabalozi pamoja na wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa mjini Vatican.