2014-01-17 14:17:30

Papa awapongeza wafanyakazi wa Vatican kwa moyo wa kujisadaka, weledi na bidii ya kazi!


Baba Mtakatifu Francisko Ijumaa, tarehe 17 Januari 2014 ameendelea kukutana na kuzungumza na wafanyakazi wanaotoa huduma ya kutayarisha na kupamba maua sehemu mbali mbali za mji wa Vatican na katika matukio ya maisha na utume wa Kanisa mjini Vatican. Hawa ni wafanyakazi wanaofanya ukarabati katika majengo ya Vatican, jambo linalohitaji moyo wa kujisadaka na uvumilivu mkuu.

Baba Mtakatifu anawapongeza kwa moyo na bidii ya kazi hasa katika kupanga viti wakati wa Ibada kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro na wakati wa Katekesi zake, kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican. Hii ni kazi inayotekelezwa kwa tija, weledi na majitoleo makubwa.

Baba Mtakatifu Francisko anawahimiza wafanyakazi wa mapambo na ukarabati kuendelea kutekeleza utume wao katika hali ya utulivu, matumaini na kusaidiana. Mwelekeo huu wa utendaji, utakuwa na tija kubwa kwa Jumuiya nzima ya wafanyakazi wa Vatican. Baba Mtakatifu amehitimisha hotuba yake kwa kuwaweka wafanyakazi pamoja na familia zao chini ya ulinzi na usimamizi wa Mtakatifu Yosefu, Mfanyakazi.








All the contents on this site are copyrighted ©.