Zaidi ya watu 200 wamefariki dunia kwa kuzama kwenye Mto Nile, jumapili iliyopita
wakati baadhi ya wananchi wa Sudan ya Kusini walipokuwa wanakimbia vita ya wenyewe
kwa wenyewe inayoendelea kupamba moto nchini humo. Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonesha
kwamba, kuna zaidi ya watu 350, 000 ambao hawana makazi kutokana na vita ya wenyewe
kwa wenyewe nchini Sudan ya Kusini.
Watu waliofariki dunia, Jumapili iliyopita
walikuwa wanatoka kwenye kitongoji cha Malakal, kilichoko Mkoa wa Upper Nile.