Chama cha Wakatekumeni Wapya kukutana na Papa Francisko, mjini Vatican, tayari kutumwa
kutangaza Injili ya Furaha!
Baba Mtakatifu Francisko, tarehe Mosi Februari 2014 anatarajiwa kukutana na Wanachama
10, 000 wa Chama cha Kitume cha Ukatekumeni Mpya mjini Vatican, kama mwanzo mpya kwa
wanachama kumi na saba kutumwa kuwatangazia watu wa Mataifa, Injili ya Furaha sehemu
mbali mbali za dunia.
Baba Mtakatifu atawaombea na kutuma Familia 75 zilizoamua
kuacha yote kwa ajili ya kutangaza Injili ya Furaha, katika miji waliyopangiwa. Familia
hizi zinaundwa na kundi la watu wanne. Kundi hili hadi wakati huu linatekeleza utume
wake katika miji 52 duniani, kwa kuwa na idadi ya familia 230. Watakapokuwa wanakutana
na Baba Mtakatifu Francisko, wadau kutoka mataifa mbali mbali wamealikwa kushiriki.